Tuesday, July 26, 2011

Kikao cha FAO chaanza rasmi mahsusi kwa eneo la Pembe ya Afrika

Ukame uliokithiri: Mifugo yafa kwa wingi na njaa imesambaa Ethiopia 

Ukame mbaya umelikumba eneo la Pembe ya Afrika na kusababisha tishio kubwa la njaa pia nchini Ethiopia. Wakati huo huo juhudi za kuyaokoa maisha ya mamilioni ya watu zitaimarishwa kwenye kikao cha FAO. 


Wajumbe wa serikali, wawakilishi wa Umoja wa Mataifa na wa mashirika ya misaada leo wanakutana mjini Rome kwa ajili ya kikao cha dharura kulijadili baa la njaa kwenye eneo la Pembe ya Afrika. Wajumbe kwenye kikao hicho wanazungumzia njia za kuwasaidia watu wapatao milioni 12 waliomo katika hatari ya kufa njaa.

Kikao hicho kinafanyika kufuatia shinikizo la kimataifa kuwataka viongozi wa dunia waongeze misaada kwa ajili ya mamilioni ya watu wanaotishiwa na baa la njaa lilisosababishwa na ukame mbaya ambao haujawahi kuonekana katika historia ya miaka 60 iliyopita katika eneo la Pembe ya Afrika. 

No comments: